Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei amesema kwamba mashambulizi ya anga ya Israel ambayo yalilenga Tehran na maeneo mengine siku ya Ijumaa usiku hayapaswi kupuuzwa wala kuonekana kuwa makubwa kuliko yalivyotokea.
Jeshi la Iran limesema kwamba wanajeshi wanne waliuawa kwenye shambulizi la anga ambalo jeshi la Israel lilisema lililenga maeneo ya kijeshi.
Khamenei amesema kwamba Israel ilifanya makosa ya kimkakati kuhusu Iran, jambo ambalo Tahran ni sharti ilifanyie kazi, kulingana na afisa aliyenukulina na kituo cha Habari cha kitaifa cha IRNA.
“Hawaifahamu vizuri Iran, “na” hawajaelewa kwa undani na vyema nguvu, uwezo na juhudi na ari ya taifa la Iran. Ni lazima tuelewe vizuri,” aliongezea.


No comments:
Post a Comment