Sunday, October 27, 2024

Chama ambacho kimekuwa madarakani kwa miaka 58, cha ahidi kufanya mabadiliko nchini Botswana

 


Na Innocent Selatlhwa akiwa Gaborone na Damiana Zane akiwa London

Chama tawala nchini Botswana – ambacho kimekuwa uongozini kwa takriban miongo sita – kinajaribu tena kutafuta ujanja wa kushinda uchaguzi mkuu wa Jumatano wiki hii kwa kutumia tamko ambalo limehusishwa kwa muda mrefu na makundi ya upinzani.

Kwenye manifesto yake, chama cha kidemokrasia cha Botswana (BDP) kinataka “mabadiliko.”

“Tufanye mabadiliko pamoja na tujenge ufanisi kwa wote,” Rais Mokgweetsi Masis – ambaye amekuwa uongozini nchini humo tangu 2018 – ameyaandika kwenye utangulizi wake.

Ni utambulizi ambao unahitaji mambo kufanyika tofauti – upinzani unasema kwamba chama cha Rais hakina uwezo wa kutimiza hilo.

Japo wachambuzi wanasema kwamba matokeo ya uchaguzi huo ni magumu kutabiri wakati huu, chama cha BDP kimeshinda viti vingi bungeni mara 11 kwenye uchaguzi mbali mbali tangu taifa hilo kunyakuwa uhuru wake 1966.

Chama hicho kimewasaidia wagombea kiti cha Urais kuingia madarakani kila mara huku wabunge wanapomchagua kiongozi wa taifa hilo.

BDP imepongezwa kwa hatua ilizochukuwa kubadilisha maisha na hali ya Uchumi wa raia katika taifa la Botswana ambalo ni masikini, na lenya hali duni ya miundombinu kama barabara chache za lami na kubadili hali ambapo maisha ya raia wa kawaida nchini humo ni ya juu kuliko kwengine kote barani Afrika.

Mojawapo ya rasilimali ambazo taifa hilo imetumia kuboresha Uchumi wake ni uchimbaji wa madini ya GEMSTONE, taifa hilo likiwa lenye kuchimba viwango vikubwa vya madini hayo kote ulimwenguni.

Na japo mambo hayako sawa.

Botswana inakabiliwa na changamoto za kiuchumi – sababu kuu ya tamko la Masisi kufanyike mabadiliko.

Kati ya watu wanne wenye uwezo wa kufanya kazi nchini humo, zaidi ya mmoja hana ajira, huku idadi kubwa ya kundi hilo likiwa vijana. Haya ni kwa mujibu wa Benki ya dunia.

Mhadhiri wa masuala ya kisiasa katika chuo kikuu cha Botswana Zibani Maundeni, ameitaja hali hiyo kama, ‘Uchumi wa watu wasiokuwa na ajira.’

‘Tunawatoa waliofuzu kwenye chuo kikuu kila mwaka na Uchumi wetu hautoi nafasi za kutosha za ajira kuwafaa wote,’ aliiambia kitengo cha LENZI KAMILI Africa Reports

Aidha, mali iliyomo nchini Botswana haijasambazwa kwa usawa miongoni mwa raia wake milioni 2.3.

1 comment:

DRC: Kambi ya rais wa zamani Joseph Kabila yapinga mradi wa kufanyia Katiba marekebisho

  Muungano wa Common Front for Congo (FCC) wa Joseph Kabila, rais wa zamani wa DRC kinapinga dhidi ya rasimu ya marekebisho ya Katiba iliyow...