Monday, October 28, 2024

DRC: Kambi ya rais wa zamani Joseph Kabila yapinga mradi wa kufanyia Katiba marekebisho

 Muungano wa Common Front for Congo (FCC) wa Joseph Kabila, rais wa zamani wa DRC kinapinga dhidi ya rasimu ya marekebisho ya Katiba iliyowasilishwa na Rais Félix Tshisekedi wiki iliyopita. 


Rais wa Kongo Félix Tshisekedi (kushoto) na mtangulizi wake Joseph Kabila (kulia) walikuwa washirika mwanzoni mwa muhula wa rais Tshisekedi. Hapa, ilikuwa Januari 24, 2019

Na: Mercy Danson  DRC



Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jioni ya Jumapili Oktoba 27, muungano wa rais wa zamani umetoa wito wa "kuzuia" mageuzi kupitia "uhamasishaji". Kambi ya Joseph Kabila pia ilitaka kufanyia marekebisho katiba mwaka 2015, na kuamua kusitisha mradi huo baada ya kupingwa na maandamlano raia na Kanisa.

Nchini DRC, muungano wa Common Front for Congo (FCC) unapinga  mradi wa marekebisho ya Katiba na kutoa "wito wa kuhamasisha raia wa Kongo" ili kuzuia mradi huo. Watu "watasimama" "kutetea haki zao", "uhuru wao", muungano wa FCC unasema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyochapishwa siku ya Jumapili jioni.

Wiki iliyopita, akiwa Kisangani, Rais Félix Tshisekedi alithibitisha nia yake ya mageuzi hayo na akataja kuanzishwa mwaka 2025 kwa tume maalum ya wataalam.

Sunday, October 27, 2024

Chama ambacho kimekuwa madarakani kwa miaka 58, cha ahidi kufanya mabadiliko nchini Botswana

 


Na Innocent Selatlhwa akiwa Gaborone na Damiana Zane akiwa London

Chama tawala nchini Botswana – ambacho kimekuwa uongozini kwa takriban miongo sita – kinajaribu tena kutafuta ujanja wa kushinda uchaguzi mkuu wa Jumatano wiki hii kwa kutumia tamko ambalo limehusishwa kwa muda mrefu na makundi ya upinzani.

Kwenye manifesto yake, chama cha kidemokrasia cha Botswana (BDP) kinataka “mabadiliko.”

“Tufanye mabadiliko pamoja na tujenge ufanisi kwa wote,” Rais Mokgweetsi Masis – ambaye amekuwa uongozini nchini humo tangu 2018 – ameyaandika kwenye utangulizi wake.

Ni utambulizi ambao unahitaji mambo kufanyika tofauti – upinzani unasema kwamba chama cha Rais hakina uwezo wa kutimiza hilo.

Japo wachambuzi wanasema kwamba matokeo ya uchaguzi huo ni magumu kutabiri wakati huu, chama cha BDP kimeshinda viti vingi bungeni mara 11 kwenye uchaguzi mbali mbali tangu taifa hilo kunyakuwa uhuru wake 1966.

Chama hicho kimewasaidia wagombea kiti cha Urais kuingia madarakani kila mara huku wabunge wanapomchagua kiongozi wa taifa hilo.

BDP imepongezwa kwa hatua ilizochukuwa kubadilisha maisha na hali ya Uchumi wa raia katika taifa la Botswana ambalo ni masikini, na lenya hali duni ya miundombinu kama barabara chache za lami na kubadili hali ambapo maisha ya raia wa kawaida nchini humo ni ya juu kuliko kwengine kote barani Afrika.

Mojawapo ya rasilimali ambazo taifa hilo imetumia kuboresha Uchumi wake ni uchimbaji wa madini ya GEMSTONE, taifa hilo likiwa lenye kuchimba viwango vikubwa vya madini hayo kote ulimwenguni.

Na japo mambo hayako sawa.

Botswana inakabiliwa na changamoto za kiuchumi – sababu kuu ya tamko la Masisi kufanyike mabadiliko.

Kati ya watu wanne wenye uwezo wa kufanya kazi nchini humo, zaidi ya mmoja hana ajira, huku idadi kubwa ya kundi hilo likiwa vijana. Haya ni kwa mujibu wa Benki ya dunia.

Mhadhiri wa masuala ya kisiasa katika chuo kikuu cha Botswana Zibani Maundeni, ameitaja hali hiyo kama, ‘Uchumi wa watu wasiokuwa na ajira.’

‘Tunawatoa waliofuzu kwenye chuo kikuu kila mwaka na Uchumi wetu hautoi nafasi za kutosha za ajira kuwafaa wote,’ aliiambia kitengo cha LENZI KAMILI Africa Reports

Aidha, mali iliyomo nchini Botswana haijasambazwa kwa usawa miongoni mwa raia wake milioni 2.3.

zilizopitaWakenya wataka mwanaharakati Boniface Mwangi kuachiliwa huru

 


Baadhi ya Wakenya wamepaza sauti wakitaka mwanaharakati Boniface Mwangi kuachiliwa huru baada ya kutekwa nyara nyumbani kwake alfajiri ya Jumapili na watu wasiojulikana.

Mke wake Njeri Mwangi amethibitisha tukio hilo kwenye akaunti yake ya mtandao wa X.

Kulingana na Njeri, Boniface alichukuliwa nyumbani na watu wasiojulikana mwendo wa saa moja asubuhi Jumapili.

Taarifa hizo zimezua hasira miongoni mwa Wakenya ambao wameilaumu serikali kwa kuhusika kwenye visa vingi vya utekaji nyara vinavyoshuhudiwa nchini Kenya.

Katika taarifa inayotazamiwa kuwa inaangazia kutekwa kwa Mwangi, aliyekuwa Rais wa chama cha mawakili nchini Kenya Eric Theuri ametaja hali ya polisi kuweka raia katika hali ya kuogopa na kuwazuia kutotoa maoni yao hadharani.

“Mapinduzi hubuniwa hivi. Matumizi ya njia zilizokuwa za kikatiba itachangia tu hali ya utawala huria.

“Visa vya watu kutekwa na matumizi ya polisi kukandamiza haki za watu kuwa na maoni kinzani na serikali kutaleta ukaidi zaidi. Siku moja, uoga utawatoka raia,’ Theuri alisema.

Mwandishi wa CNN Larry Madowo amezungumzia suala hilo kwa kusema kwamba visa vya utekaji nyara vimeendelea kuwanasa na kuwakandamiza wanaharakati na wapinzani wakuu wa serikali japo serikali imekanusha kuhusika.

“Mwanaharakati kutoka Kenya ametekwa nyara na watu wasiojulikana.#FreeBonifaceMwangi,” Alisema Larry Madowo kwenye Mtandao wa X.

Mwandishi mpekuzi John Allan Namu pia amezungumzia suala la ubakaji kwenye mtandao wa X : “ Hili linapaswa kukoma. #FreeBonifaceMwangi”.

Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali yamelaani kutekwa kwa Mwangi.

Social centres working group wameshutumu kitendo hicho pia na kusema:

“Tunalaani vikali kitendo hicho kilichotekelezwa na maafisa wa serikali. Mwangi ni mwanaharakati wa haki za kibinadamu ambaye hajakosa kutekeleza majukumu yake ipasavyo, alikuwa amepanga kuhudhuria mbio za Standard Chartered Marathon. Kuzuiliwa kwa Mwangi kinyume na sheria ni jambo la kuhuzunisha na kukiuka uhuru wa kujieleza. #FreeBonifaceMwangi

Kundi la The Defenders Coalition kwa upande wake limetaja hatua hiyo ya Mwangi kutekwa kama ukiukaji mkubwa wa haki zake za kibinadamu wakiongezea kwamba uchokozi wa aina hiyo hautakubalika.

Hata hiyo, polisi imetoa taarifa na kusema wanamzuilia katika kituo cha polisi cha Kamukunji jijini Nairobi

Mashambulizi ya Israel hayapaswi kupuuzwa, asema kiongozi mkuu wa Iran

 


Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei amesema kwamba mashambulizi ya anga ya Israel ambayo yalilenga Tehran na maeneo mengine siku ya Ijumaa usiku hayapaswi kupuuzwa wala kuonekana kuwa makubwa kuliko yalivyotokea.

Jeshi la Iran limesema kwamba wanajeshi wanne waliuawa kwenye shambulizi la anga ambalo jeshi la Israel lilisema lililenga maeneo ya kijeshi.

Khamenei amesema kwamba Israel ilifanya makosa ya kimkakati kuhusu Iran, jambo ambalo Tahran ni sharti ilifanyie kazi, kulingana na afisa aliyenukulina na kituo cha Habari cha kitaifa cha IRNA.

“Hawaifahamu vizuri Iran, “na” hawajaelewa kwa undani na vyema nguvu, uwezo na juhudi na ari ya taifa la Iran. Ni lazima tuelewe vizuri,” aliongezea.

Wanane wauawa kwenye shambulizi la Israel, yasema wizara ya afya ya Lebanon


Moshi unafuka angani baada ya shambulizi la Israel huko Sidon.

Wimbi jipya la Mauaji ya Halaiki Sudan kuchukua Sura mpya

  M


kuu wa umoja wa mataifa nchini Sudan amesema kwamba ametiwa wasiwasi mkubwa na ripoti za madhila makubwa ya kihalifu yanayotekelezwa katika jimbo la kati nchini Sudan la Gezira, ikiwemo mauaji ya halaiki ya raia yanayotekelezwa na kikosi maalum cha wanamgambo cha Rapid Support Force RSF.

Clementine Nkweta-Salami ametoa matamshi yake baada ya kundi la wanaharakati kusema kwamba watu 124 wameuawa na kikosi cha RSF kwenye mashambulizi yaliyotekelezwa kwenye vijiji katika wiki moja iliyopita.

RSF imekanusha shutuma hizo kwamba inawalenga raia, ikisema kwamba wapiganaji wake wanakabiliana na waasi waliopewa silaha na jeshi la Sudan.

Mzozo huo ambao umeendelea kwa miezi 18 sasa umesababisha vifo vya maelfu ya watu na kuwalazimisha wengine milioni 11 kuhama makwao.

Nkweta-Salam , ambaye ni msimamizi wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa mataifa nchini Sudan, amesema kwamba taarifa za awali zimeashiria kwamba RSF ilitekeleza mashambulizi mawili katika maeneo tofauti kwenye jimbo la Gezira kati ya Oktoba 20 na 25, 2024.

Aidha amesema kwamba hali hiyo ilichangia maafa ya watu wengi na kuwa shambulizi la halaiki, huku wanawake wakibakwa, nazo biashara zikiporwa na wengine kupora mali ya watu kwenye makazi ya kibinafsi na hata kuchoma mashamba ya watu.

Bi Nkweta - Salam amesema kwamba maovu hayo ya kihalifu ni saw ana kilichoshuhudiwa katika jimbo la Darfur mwaka wa 2023, wakati ambapo RSF ilishutumiwa kwa kutekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya jamii ambazo zilionekana kupinga kikosi hicho.

Nkweta Salam, aidha amesema kwamba idadi kamili ya waliofariki haijulikani, lakini taarifa za awali zimeonyesha kwamba wengi waliuawa katika jimbo la Gezira.

Iran yasema azma yake ya kujilinda haina kikomo

 Iran yasema azma yake ya kujilinda haina kikomo


Azma ya Iran ya kujilinda "h


aina kikomo", Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema siku ya Jumamosi Oktoba 26, 2024, baada ya mashambulizi ya usiku ya Israel dhidi ya maeneo ya kijeshi ya nchi hiyo.

DRC: Kambi ya rais wa zamani Joseph Kabila yapinga mradi wa kufanyia Katiba marekebisho

  Muungano wa Common Front for Congo (FCC) wa Joseph Kabila, rais wa zamani wa DRC kinapinga dhidi ya rasimu ya marekebisho ya Katiba iliyow...